utangulizi
Himdi zote zinamstahikia Allaah Mmoja. Swalah na salaam zimwendee mja na Mtume Wake, Mtume wetu Muhammad, kizazi chake na Maswahabah zake.
Amma ba´d:
Haya ni maneno mafupi yenye kubainisha namna ya swalah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Nimependa kuwawakilishia nayo waislamu wote wanaume kwa wanawake ili kila yule atakayeisoma aweze kumuiga (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika hilo. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
"Swali kama mlivyoniona nikiswali."
Ameipokea al-Bukhaariy.