Namna ya kukaa Tashahhud katika Rakaa´ ya tatu na ya nne
Namna ya kukaa Tashahhud katika Rakaa´ ya tatu na ya nne
14- Ikiwa swalah ni ya Rakaa´ tatu, kama Maghrib, au ya Rakaa´ nne kama Dhuhr, ´Aswr na ´Ishaa atasoma Tashahhud iliyotanguliwa kutajwa punde tu [baada ya Rakaa´ mbili] pamoja na kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) halafu atasimama hali ya kujisaidiza kwa kushika mapaja yake na wakati huo huo ainyanyue mikono yake sawa na mabega yake na huku aseme
"Allaahu Akbar" na aiweke mikono yake juu ya kifua chake - kama tulivyotangulia hapo juu - na asome "al-Faatihah" peke yake. Baadhi ya nyakati katika swalah za Rakaa´ tatu na nne baada ya kusoma "al-Faatihah"
akisoma Suurah nyingine ni sawa. Kumethibiti yanayofahamisha hivo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupitia Hadiyth ya Abu Sa´iyd (Radhiya Allaahu ´anh). Endapo ataacha kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya Tashahhud ya kwanza ni sawa. Kwa sababu imependekezwa na sio jambo la wajibu katika Tashahhud ya kwanza.
Baada ya Rakaa´ ya tatu atakaa Tashahhud [ya mwisho] ikiwa ni Maghrib na [atakaa Tashahhud] baada ya Rakaa´ ya nne ikiwa ni Dhuhr, ´Aswr na ´Ishaa - kama ilivyotangulia katika swalah za Rakaa´ mbili - kisha amswalie Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na aombe kinga kutokamana na adhabu ya Moto, kaburi, fitina ya al-Masiyh ad-Dajjaal na akithirishe kuomba du´aa, kama yalivyotangulia hayo katika swalah ya Rakaa´ mbili. Lakini katika kikao hichi anatakiwa kukaa kitako cha Tawarruk. Nacho ni kuuweka mguu wake wa kushoto chini ya mguu wake wa kulia na makalio yake ayakaze juu ya ardhi
na wakati huo huo mguu wake wa kulia awe ameusimamisha kutokamana na"as-Salaam ´alaykum wa Rahmatullaah."
Halafu amuombe Allaah maghfirah mara tatu. Baada ya hapo atasema:
} ال نت ال لام منك ال لام تبا كت ا الجلال الإك ام {
"Allaahumma antas-Salaam, wa minkas-Salaam, tabaarakta yaadhal-Jalaal wal-Ikraam."
"Ee Allaah! Hakika Wewe ndiye as-Salaam, amani inatoka Kwako, umetukuka ewe Mwenye utukufu na Mwenye kustahilki kuheshimika." (Muslim (591), at-Tirmidhiy (300), Abu Daawuud (1512), Ibn Maajah (928), Ahmad (05/280) na ad-Daarimiy (1348).)
kabla ya kuwaelekea watu iwapo atakuwa ni imamu. Kisha aseme:
} لا لو لا ا ه للّ حده لا ش يك لو، لو الم ك لو الح د ى ع ى كل شي دي ، ال لا مانع لما عطيت لا معطي لما منعت لا ينفع ا
الجد منك الجد، لا ح ل لا ة لا بالله، لا لو لا ا ه للّ لا نعبد لا ه لو النع ة لو الفضل لو الثنا الح ن لا لو لا ا ه للّ مخ ل لوالدين ل ك ه ال ا ن {
"Laa ilaaha illa Allaah, wahdahuu laa shariyka lah, lahul-Mulk wa lahul-Hamd wa huwaa ´alaa kulli shay-in Qadiyr. Laa hawla wa laa quwwatah illa billaah. Allaahumma laa maaniy´ limaa a´twayt, wa laa mu´twiya limaa mana´t, wa laa yanfau´ dhal jaddi mink al-Jadd. Laa hawla wa laa quwwatah illa billaah, laa ilaaha illa Allaah, wa laa na´abudu illa iyyaah, lahun-Ni´mah wa lahul- Fadhwl, wa lahuth-Thanaa´ al-Hasan. Laa ilaaha illa Allaah, mukhliswiyna lahud-Diyn, wa lau karihal-Kaafiruun."
"Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah, hali ya kuwa peke yake hana mshirika, ufalme ni wa Kwake na himdi ni Zake Naye juu ya kila jambo ni muweza. Hakuna nguvu wala uwezo isipokuwa kwa msaada wa Allaah. Ee Allaah! Hapana awezae kukizuia ulichokitoa na kukitoa ulichokizuia - wala haumnufaishi mwenye utajiri, kwani Kwako wewe ndio utajiri. Hakuna nguvu wala uwezo isipokuwa kwa msaada wa Allaah, hatumuabudu mwengine asiyekuwa Yeye, neema na fadhila na sifa nzuri zote ni Zake. Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah, hali ya kumtakasia Yeye dini ijapokuwa watachukia makafiri." (al-Bukhaariy (808), Muslim (593), an-Nasaa´iy (1341), Abu Daawuud (1505), Ahmad (04/250) na ad-Daarimiy (1349).)
"Laa ilaaha illa Allaah illa Allaah, wahdahuu laa shariyka lah, a wa lahul- Hamd wa huwaa ´alaa kulli shay-in Qadiyr." Baada ya hapo asome Aayat-ul- Kursiy, Suurah "al-Ikhlaasw", "al-Falaq" na "an-Naas". Afanye hivi baada ya kila swalah. Imependekezwa kukariri Suurah hizi mara tatu-tatu baada ya swalah ya Fajr na Maghrib. Kumepokelewa Hadiyth juu ya hayo kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Adhkaar zote hizi ni Sunnah na sio faradhi.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akizihifadhi katika hali isiyokuwa ya usafiri. Kuhusu anapokuwa katika hali ya usafiri alikuwa haziswali isipokuwa Sunnah ya Fajr na Witr. Hakika hizi mbili Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akizihifadhi katika anapokuwa safarini na
asipokuwa safarini. Lililo bora ni kuziswali Raatibah hizi na Witr nyumbani.Lakini hata hivyo akiziswali msikitini pia ni sawa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Swalah bora ya mtu ni ile anayoswali nyumbani kwake isipokuwa zile za faradhi." (al-Bukhaariy (689), Muslim (1301) na at-Tirmidhiy (412).)
Kuhifadhi swalah hizi ni miongoni mwa sababu zinazompelekea mtu kuingia Peponi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Anayeswali Rakaa´ kumi na mbili mchana na usiku, basi Allaah atamjengea nyumba Peponi." (Muslim (1198-1199), Abu Daawuud (1059) na an-Nasaa´iy (1773).)
Endapo ataswali Rakaa´ nne kabla ya ´Aswr, Rakaa´ mbili kabla ya Maghrib na Rakaa´ mbili kabla ya ´Ishaa ni jambo zuri. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
"Atakayehifadhi Rakaa´ nne kabla ya Dhuhr na Rakaa´ nne baada yake, basi Allaah (Ta´ala) atamharamishia Moto."(at-Tirmidhiy (393), Abu Daawuud (1077) na Ahmad (25547).)
Ina maana ya kwamba akizidisha Rakaa´ mbili baada ya Dhuhr - kwa sababu Sunnah ya Raatibah ni nne kabla yake na mbili baada yake - basi atakuwa amefikia kile kilichotajwa katika Hadiyth ya Umm Habiybah (Radhiya Allaahu ´anhaa). Allaah ndiye anayeongoza katika mafanikio.
Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad bin ´Abdillaah, kizazi chake na Maswahabah zake na wenye kuwafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah