Namna ya kukaa baina ya Sijdah mbili
Namna ya kukaa baina ya Sijdah mbili
10- Anyanyue kichwa chake na huku akisema "Allaahu Akbar" na auinamishe mguu wake wa kushoto na auikalie na wakati huo huo asimamishe mguu wa kulia na aweke mikono yake juu ya mapaja na magoti yake na aseme:
Anatakiwa awe na utulivu katika kikao hichi.
11- Asujudu Sijda ya pili na huku akisema "Allaahu Akbar" kisha afanye yale yale aliyofanya katika Sajdah ya kwanza.
12- Ainue kichwa chake na huku akisema "Allaahu Akbar" na akae kikao khafifu kama mfano wa kikao baina ya Sajdah mbili. Hiki huitwa kuwa ni "kikao cha kustarehe" ambacho kimependekezwa kwa mujibu wa maoni sahihi ya wanachuoni. Endapo atakiacha hakuna neno. Katika kikao hichi hakuna Dhikr wala du´aa. Kisha asimame/apande kwenda katika Rakaa´ ya pili hali ya kujisaidiza kwa kushika mapaja - ikiwa kuna urahisi wa kufanya hivo - lasivyo ajisaidize kwa ardhi. Halafu asome "al-Faatihah" na kilicho chepesi kwake katika Qur-aan baada ya al-Faatihah. Ataendelea kufanya kama alivyofanya katika Rakaa´ ya kwanza.